
MKULAZI HOLDING COMPANY LIMITED

Wajumbe wa Bodi ya Kampuni Hodhi ya Mkulazi wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dkt. Hildelitha Msita wametembelea na kukagua miundombinu ya umwagiliaji katika Shamba la Miwa Mbigiri pamoja na kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha sukari April 13, 2023.
Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Taifa wa Hifadhi ya jamii (NSSF) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Ali Idi Siwa wamefanya ziara ya kikazi kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha Sukari kilichopo Mbigiri Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro Machi 20, 2023.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Daniel Chongolo ameridhishwa na hatua iliyofikiwa ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha sukari kilichopo Mbigiri Wilaya ya Kilosa Mkoa wa Morogoro mara baada ya kutembelea ujenzi wa kiwanda hicho akiongozana na Viongozi wengine wa Chama hicho.
Ameyasema hayo Januari 30,2023 wakati akizungumza na ...