
MKULAZI HOLDING COMPANY LIMITED

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)Taifa Daniel Chongolo akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni Hodhi ya Mkulazi Dkt. Hildelitha Msita wakati alipowasili katika Makao Makuu ya Ofisi ya Kampuni hiyo wakati alipofanya ziara ya kutembelea utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kiwanda Januari mwaka huu .
Serikali imehimiza mkandarasi anayesimamamia kazi ya ujenzi Kiwanda cha Sukari Mkulazi kufanya kazi hiyo ndani ya muda ulioweka kwenye Mkataba.
Ujenzi Kiwanda cha Sukari Mbigiri kilichopo wilaya ya Kilosa Mkaoni Morogoro umefikia asilimia 55 ambapo kinatarajiwa kuanza kuzalisha sukari hivi karibuni. Kiwanda hicho kina ukubwa wa eneo la hekta 4,856, kati ya hizo eneo la hekta 3,600 zitalimwa na kupandwa miwa. Tayari eneo lenye ukubwa wa hekta 2,810 limeshapandwa miwa ambalo ni sawa na ...